E aniquilamos o povo de Ad e o de Samud, como atestam (as ruínas de) suas casas, porque Satanás lhes abrilhantou asações e os desencaminhou da (verdadeira) senda, apesar de serem perspicazes.
Tafsirs
Camadas
Lições
Reflexões
Respostas
Qiraat
Hadith
Na tukawaangamiza kina 'Ād na Thamūd, na yameshaonekana na nyinyi magofu ya nyumba zao, vile yalivyokuwa matupu, hayana mtu yoyote katika wakazi wake, na vile mateso yetu yalivyowashukia wao wote. Na Shetani aliwapambia wao matendo yao maovu, na kwa hivyo akawazuia wasiifuate njia ya Mwenyezi Mungu na njia ya kumuamini Yeye na Mitume Wake, na walikuwa wakijiongoza kuona njia katika ukafiri wao na upotevu wao wakijifurahisha nayo, wakidhani kwamba wao wako kwenye uongofu na usawa, ilhali wao wamezama kwenye upotevu.