São aqueles que, quando os estabelecemos na terra, observam a oração, pagam o zakat, recomendam o bem e proíbem oilícito. E em Deus repousa o destino de todos os assuntos.
Tafsirs
Camadas
Lições
Reflexões
Respostas
Qiraat
Hadith
Wale tuliowaahidi kuwa tutawanusuru ndio wale tukiwapa utulivu kwenye ardhi na kuwatawalisha humo kwa kuwapa ushindi juu ya adui wao, wanasimamisha Swala kwa kuiitekeleza kwa nyakati zake kwa namna zake, wanatoa Zaka za mali zao kuwapa wastahiki wake, wanaamrisha kila ambalo Mwenyezi Mungu Ameliamrisha la haki Zake na haki za waja Wake na wanakataza kila ambalo Mwenyezi Mungu Amelikataza na Mtume Wake. Na ni wa Mwenyezi Mungu Peke Yake mwisho wa mambo yote, na mwisho mwema ni wa uchamungu.