Estão jubilosos por tudo quanto Deus lhes concedeu da Sua graça, e se regozijam por aqueles que ainda nãosucumbiram, porque estes não serão presas do temor, nem se atribularão.
Tafsirs
Camadas
Lições
Reflexões
Respostas
Qiraat
Hadith
Furaha iliwaenea, wakati Mola wao Alipowaneemesha na kuwapa neema na radhi zenye kuwaliwaza macho yao, zikiwa ni miongoni mwa ukarimu Wake na takrima Yake. Watakuwa wakiwafurahia ndugu zao wenye kupigana jihadi waliowaacha duniani wakiwa hai, wakiwatarajia wafaulu kama walivyofaulu wao. Kwa kuwa wao waelewa kwamba hao ndugu zao, waliowaacha duniani wakiwa hai, watapata heri waliyoipata wao, iwapo watakufa mashahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu hali ya kumtakasia Yeye, na kwamba hawatakuwa na chochote cha kuogopa kuhusu mambo ya mustakbali wao huku Akhera wanayoyakabili wala hawatakuwa na huzuni juu ya yale yaliyowapita wakayakosa ya hadhi za kilimwengu.