Оно плодоносит каждый миг с дозволения своего Господа. Аллах приводит людям притчи, - быть может, они помянут назидание.
Тафсиры
Слои
Уроки
Размышления
Ответы
Кираат
Хадис
Unatoa matunda yake kila kipindi kwa idhini ya Mola wake. Namna hiyo ndivyo ulivyo mti wa Imani: msingi wake umejikita imara ndani ya moyo wa Muumini kiujuzi na kiitikadi, na tagaa zake za matendo mema na tabia za kuridhisha zinapaishwa juu kwa Mwenyezi Mungu, na malipo yake mema yanapatikana kila kipindi. Na Mwenyezi Mungu Anawapigia watu mfano ili wakumbuke na wawaidhike wapate kuzingatia.