Кто может быть несправедливее того, кто возвел навет на Аллаха и счел ложью правду, когда она явилась ему? Разве не в Геенне обитель неверующих?
Тафсиры
Слои
Уроки
Размышления
Ответы
Кираат
Хадис
Hakuna yoyote dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzulia Mwenyezi Mungu urongo, kwa kumnasibishia sifa isiyofaa kusifika nayo, kama vile kuwa na mshirika na mtoto, au akasema, «Mimi nimeletewa wahyi,» na hali yeye hakuletewa wahyi wa kitu chochote. Na hakuna dhalimu zaidi kuliko yule aliyeikanusha haki iliyoteremka kwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Kwani si yako huko Motoni mashukio na makazi kwa waliomkufuru Mwenyezi Mungu na wasimuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie? Ndio, yako.