A thua çdoherë që japin ndonjë premtim, disa prej tyre e flakin tej atë? Jo, por shumica e tyre nuk besojnë.
Tefsiret
Shtresat
Mësimet
Reflektime
Përgjigjet
Kiraat
Hadith
Ni ubaya ulioje wa hali ya Wana wa Isrāīl katika kuvunja kwao ahadi! Kila wanapotoa ahadi, kinatoka kikundi cha watu katika wao wakaitupa na wakaivunja. Utawaona wanaifunga ahadi leo na kuitangua kesho. Bali wengi wao hawayaamini aliyokuja nayo Nabii wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake Muhammad, rehema na amani zimshukiye yeye.