O besimtarë! Në të vërtetë, ju keni armiq në radhët e grave tuaja dhe të fëmijëve tuaj, andaj ruajuni prej tyre! Por, nëse nuk i vini re fyerjet e tyre dhe ua falni, ta dini se Allahu është vërtet Falës dhe Mëshirëplotë1.
Tefsiret
Shtresat
Mësimet
Reflektime
Përgjigjet
Kiraat
Hadith
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake! Kwa kweli miongoni mwa wake zenu na wana wenu ni maadui wenu, wanawazuia nyinyi na njia ya Mwenyezi Mungu na wanawavunja moyo ya kumtii Mwenyezi Mungu, basi jihadharini nao wala msiwasikilize. Na iwapo mtayasamehe makosa yao, mkayapa mgongo na mkayaficha msiyatangaze, basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe ni Mwingi wa rehema, Atawasamehe nyinyi madhambi yenu, kwani Yeye, Aliyetakasika na kila upungufu, ni Mkubwa wa kusamehe ni Mkunjufu wa rehema.