Sema: Ameiteremsha hii Roho takatifu kutokana na Mola wako Mlezi kwa haki, ili awathibitishe wale walio amini, na kuwa ni uwongofu, na ni bishara kwa Waislamu. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Waambie, ewe Mtume, Qurani haikuzuliwa na mimi, bali aliyeiteremsha ni Jibrili kutoka kwa Mola wako kwa ukweli na uadilifu ili kuwafanya Waumini wawe imara, kuwaongoza wao kutoka kwenye upotevu , na kuwapa bishara njema wale waliojisalimisha na kunyenyekea kwa Mwenyezi Mungu, Bwana wa viumbe wote.