Hakika Mwenyezi Mungu amewafanyia wema mkubwa Waumini vile alivyo waletea Mtume aliye miongoni mwao wenyewe, anaye wasomea Aya zake, na anawatakasa, na anawafunza Kitabu na hikima, ijapo kuwa kabla ya hapo walikuwa katika upotovu ulio wazi. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Hakika Mwenyezi Mungu Amewapa neema Waumini, miongoni mwa Waarabu, Alipomtumiliza Mtume atokaye katika jinsi yao, akawa anawasomea wao aya za Qur’ani, anawatakasa na ushirikina na tabia mbaya na anawafundisha Qur’ani na Suna, pamoja na kwamba kabla ya Mtume huyu walikuwa kwenye upotevu na ujinga ulio wazi.