Ingia
Ingia
Ingia
Chagua Lugha

Tafsir: Aali-Imran 3:73

3:73
ولا تومنوا الا لمن تبع دينكم قل ان الهدى هدى الله ان يوتى احد مثل ما اوتيتم او يحاجوكم عند ربكم قل ان الفضل بيد الله يوتيه من يشاء والله واسع عليم ٧٣
وَلَا تُؤْمِنُوٓا۟ إِلَّا لِمَن تَبِعَ دِينَكُمْ قُلْ إِنَّ ٱلْهُدَىٰ هُدَى ٱللَّهِ أَن يُؤْتَىٰٓ أَحَدٌۭ مِّثْلَ مَآ أُوتِيتُمْ أَوْ يُحَآجُّوكُمْ عِندَ رَبِّكُمْ ۗ قُلْ إِنَّ ٱلْفَضْلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤْتِيهِ مَن يَشَآءُ ۗ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٌۭ ٧٣
وَلَا
تُؤۡمِنُوٓاْ
إِلَّا
لِمَن
تَبِعَ
دِينَكُمۡ
قُلۡ
إِنَّ
ٱلۡهُدَىٰ
هُدَى
ٱللَّهِ
أَن
يُؤۡتَىٰٓ
أَحَدٞ
مِّثۡلَ
مَآ
أُوتِيتُمۡ
أَوۡ
يُحَآجُّوكُمۡ
عِندَ
رَبِّكُمۡۗ
قُلۡ
إِنَّ
ٱلۡفَضۡلَ
بِيَدِ
ٱللَّهِ
يُؤۡتِيهِ
مَن
يَشَآءُۗ
وَٱللَّهُ
وَٰسِعٌ
عَلِيمٞ
٧٣
Wala msimuamini ila anaye fuata dini yenu. Sema: Hakika uwongofu ni uwongofu wa Mwenyezi Mungu, kuwa apewe mtu mfano wa mlio pewa nyinyi au wakuhojini mbele ya Mola wenu Mlezi. Sema: Hakika fadhila zimo mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa na Mjuzi. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
«Na msimsadiki kikweli isipokuwa yule aliyefuata dini yenu akawa Myahudi.» Waambie, ewe Mtume, «Uongofu na taufiki ni uongofu wa Mwenyezi- Mungu na taufiki Yake ya kuongoza kwenye Imani sahihi.» Na walisema, «Msiidhihirishe kwa Waislamu elimu mlionayo, wasije wakajifunza kutoka kwenu wakawa sawa na nyinyi katika kuijua na wakawa na ubora juu yenu au wakaichukua kuwa ni hoja kutoka kwa Mola wenu wakawashinda kwayo.» Waambie, ewe Mtume, «Fadhila na vipawa na mambo yote yako mkononi mwa Mwenyezi Mungu na yako chini ya uendeshaji Wake, Anampa Amtakaye miongoni mwa waliomuamini Yeye na Mtume Wake. Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu na ni Mjuzi: Anawaenea, kwa elimu Yake na upaji Wake, viumbe Vyake vyote vinavyostahiki fadhila Zake na neema Zake.»