Ingia
Ingia
Ingia
Chagua Lugha

Tafsir: Al-Aaraf 7:58

7:58
والبلد الطيب يخرج نباته باذن ربه والذي خبث لا يخرج الا نكدا كذالك نصرف الايات لقوم يشكرون ٥٨
وَٱلْبَلَدُ ٱلطَّيِّبُ يَخْرُجُ نَبَاتُهُۥ بِإِذْنِ رَبِّهِۦ ۖ وَٱلَّذِى خَبُثَ لَا يَخْرُجُ إِلَّا نَكِدًۭا ۚ كَذَٰلِكَ نُصَرِّفُ ٱلْـَٔايَـٰتِ لِقَوْمٍۢ يَشْكُرُونَ ٥٨
وَٱلۡبَلَدُ
ٱلطَّيِّبُ
يَخۡرُجُ
نَبَاتُهُۥ
بِإِذۡنِ
رَبِّهِۦۖ
وَٱلَّذِي
خَبُثَ
لَا
يَخۡرُجُ
إِلَّا
نَكِدٗاۚ
كَذَٰلِكَ
نُصَرِّفُ
ٱلۡأٓيَٰتِ
لِقَوۡمٖ
يَشۡكُرُونَ
٥٨
Na ardhi njema, yenye udongo wa rutba, hutoa mimea yenye kukua vizuri yenye uhai, kwa idhini ya Mola Mlezi wake. Na ardhi mbaya haitoi ila mimea michache, isiyo na faida, tena kwa shida. Na hivyo ndivyo tunavyo zipambanua Ishara (Aya) kwa watu wanao shukuru. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Na ardhi nzuri, ikiteremkiwa na mvua, inatoa mimea kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na matakwa Yake, ikiwa mizuri na kwa njia ya wepesi. Hivyo ndivyo alivyo Muumini, zikiteremka aya za Mwenyezi Mungu kwake, hunufaika nazo na huzalisha kwake maisha mema. Ama ardhi ya chumvi iliyo mbovu; hiyo haitoi mimea isipokuwa mibovu isiyokuwa na faida, tena kwa shida, na haitoi mimea mizuri. Hivyo ndivyo alivyo kafiri, hanufaiki kwa aya za Mwenyezi Mungu. Mfano wa sampuli hiyo nzuri katika kueleza, ndiyo namna tunavyoleta hoja na dalili mbalimbali kuthibitisha haki kwa watu wanaozishukuru neema za Mwenyezi Mungu na wanaomtii.