Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka khamsini. Basi tufani liliwachukua, nao ni madhaalimu.
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Na hakika tulimtumiliza Nūḥ kwa watu wake, akakaa kwao miaka elfu moja kasoro miaka hamsini, akiwaita kwenye upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na akiwakataza ushirikina, na wao wasimuitikie. Mwenyezi Mungu Akawaangamiza kwa mafuriko, na wao wako katika hali ya kujidhulumu wenyewe kwa ukafiri wao na kupita kiasi kwao katika uasi.