Anaingiza usiku katika mchana, na anaingiza mchana katika usiku. Na Yeye ni Mwenye kuyajua yaliomo vifuani.
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Anazitia saa za usiku zilizopungua ndani ya mchana na hivyo basi mchana ukaongezeka, na Anazitia saa za mchana ndani ya usiku, na hivyo basi usiku ukaongezeka. Na Yeye , kutakasika ni Kwake, ni Mjuzi wa yaliyomo ndani ya vifua vya viumbe Vyake.