Ingia
Ingia
Ingia
Chagua Lugha

Tafsir: Al-Hajj 22:41

22:41
الذين ان مكناهم في الارض اقاموا الصلاة واتوا الزكاة وامروا بالمعروف ونهوا عن المنكر ولله عاقبة الامور ٤١
ٱلَّذِينَ إِن مَّكَّنَّـٰهُمْ فِى ٱلْأَرْضِ أَقَامُوا۟ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَوُا۟ ٱلزَّكَوٰةَ وَأَمَرُوا۟ بِٱلْمَعْرُوفِ وَنَهَوْا۟ عَنِ ٱلْمُنكَرِ ۗ وَلِلَّهِ عَـٰقِبَةُ ٱلْأُمُورِ ٤١
ٱلَّذِينَ
إِن
مَّكَّنَّٰهُمۡ
فِي
ٱلۡأَرۡضِ
أَقَامُواْ
ٱلصَّلَوٰةَ
وَءَاتَوُاْ
ٱلزَّكَوٰةَ
وَأَمَرُواْ
بِٱلۡمَعۡرُوفِ
وَنَهَوۡاْ
عَنِ
ٱلۡمُنكَرِۗ
وَلِلَّهِ
عَٰقِبَةُ
ٱلۡأُمُورِ
٤١
Wale ambao tukiwapa madaraka katika nchi husimamisha Swala, na wakatoa Zaka, na wakaamrisha mema, na wakakataza mabaya. Na kwa Mwenyezi Mungu ndio marejeo ya mambo yote. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Wale tuliowaahidi kuwa tutawanusuru ndio wale tukiwapa utulivu kwenye ardhi na kuwatawalisha humo kwa kuwapa ushindi juu ya adui wao, wanasimamisha Swala kwa kuiitekeleza kwa nyakati zake kwa namna zake, wanatoa Zaka za mali zao kuwapa wastahiki wake, wanaamrisha kila ambalo Mwenyezi Mungu Ameliamrisha la haki Zake na haki za waja Wake na wanakataza kila ambalo Mwenyezi Mungu Amelikataza na Mtume Wake. Na ni wa Mwenyezi Mungu Peke Yake mwisho wa mambo yote, na mwisho mwema ni wa uchamungu.