Je! Huwaoni wale wanao bishana katika Ishara za Mwenyezi Mungu? Wanageuziwa wapi?
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Je, huwaonei ajabu, ewe Mtume, hawa wakanushaji wa aya za Mwenyezi Mungu vile wanavyoshindana nazo, na hali hizo ziko wazi katika kutolea ushahidi upweke wa Mwenyezi Mungu na uweza Wake, ni vipi wao wanaziepuka pamoja na usahihi wake? Na wataenda kwenye kitu gani baada ya huu ufafanuzi kamili?