Wala hawalingani walio hai na maiti. Hakika Mwenyezi Mungu humsikilizisha amtakaye. Wala wewe si wa kuwasikilizisha walio makaburini.
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Na wale waliohuika nyoyo kwa kukuamini hawalingani na wale waliokufa nyoyo kwa kukanusha. Hakika Mwenyezi Mungu Anamsikilizisha Anayemtaka asikie kwa kufahamu na kukubali. Na wewe, ewe Mtume, si mwenye kuwasikilizisha walio ndani ya makaburi. Na kama usivyoweza kuwasikilizisha wafu makaburini mwao, pia hutawasikilizisha hawa makafiri kwa kuwa nyoyo zao zimekufa.