Kama yaliyo wapata watu wa Firauni na wale walio kuwa kabla yao. Walikanusha Ishara zetu, basi Mwenyezi Mungu aliwashika kwa madhambi yao; na Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Hali ya makafiri katika kukanusha kwao na adhabu itakayowashukia ni kama hali ya jamaa za Fir’aun na wale makafiri waliokuwa kabla yao. Wao walizikanusha aya za Mwenyezi Mungu zilizo wazi, Mwenyezi Mungu akawapatiliza kwa kuwatesa kwa sababu ya kukanusha kwao na kushindana. Na Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kutesa kwa aliyemkufuru Yeye na kuwakanusha Mitume Wake.