Pale pale Zakariya akamwomba Mola wake Mlezi, akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe kutoka kwako uzao mwema. Wewe ndiye unaye sikia maombi. 1
Tafsir
Tabaka
Mafunzo
Tafakari
Majibu
Qiraat
Hadith
Alipoona Zakariyyā vile Mwenyezi Mungu Alivyomkirimu Maryam kwa riziki Yake na fadhila Zake, alielekea kwa Mola wake akisema, «Ewe Mola wangu, nipe kutoka Kwako mtoto mwema mwenye kubarikiwa. Wewe ni Msikizi wa maombi ya anayekuomba.»