Enyi watu wa Taurati na Injili! Vipi nyinyi mnakanusha aya za Mwenyezi Mungu ambazo aliziteremsha kwa Mitume wake katika Vitabu vyenu, na ndani yake muna kuwa Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ndiye Mtume anayengojewa na kuwa aliyowajia nayo ndio haki. Na nyinyi mnashuhudia hilo, lakini mnalikanusha.