Na makafiri wa Makkah wanasema, «Basi si ajiwe na miujiza inayoonekana kama fimbo ya Mūsā na ngamia wa Ṣāliḥ.» Na hilo haliko kwenye mkono wako, ewe Mtume; hukuwa wewe isipokuwa ni mwenye kuwafikishia na ni mwenye kuwatisha adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na kila ummah una mjumbe wa kuwaongoza kwenye njia ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.