Vaktaki Allah katından onlara, kendilerinde olanı tasdik eden Kitap geldi ki onlar bundan önceleri, inkar edenlere karşı kendilerine yardım gelmesini beklerlerdi, bildikleri gelince onu inkar ettiler. Allah'ın laneti, inkar edenlerin üzerine olsun.
Tefsirler
Katmanlar
Dersler
Yansımalar
Cevaplar
Kıraat
Hadis
Na ilipowajia Qur’ani inayotoka kwa Mwenyezi Mungu, ikisadikisha yale ambayo waliokuwa nayo kwenye Taurati, waliikanusha na kuukataa utume wa Muhammad, rehema na mani zimshukie. Na walikuwa, kabla ya kutumilizwa kwake, wakitumai kusaidiwa na yeye dhidhi ya washirikina wa Kiarabu, na walikuwa wakisema, “Umekaribia wakati wa kutumilizwa Mtume wa zama za mwisho ambaye sisi tutamfuata na tutapigana na nyinyi tukiwa pamoja na yeye.” Alipowajia huyo Mtume, ambaye walizijua sifa zake na ukweli wake, walimkataa na walimkanusha. Basi laana ya Mwenyezi Mungu imshukie kila aliyemkanusha Nabii na Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad, rehema na amani zimshukie, na kukanusha Kitabu chake ambacho Mwenyezi Mungu alimletea kwa njia ya Wahyi.