وكتبنا عليهم فيها ان النفس بالنفس والعين بالعين والانف بالانف والاذن بالاذن والسن بالسن والجروح قصاص فمن تصدق به فهو كفارة له ومن لم يحكم بما انزل الله فاولايك هم الظالمون ٤٥
Orada onlara cana can, göze göz, buruna burun, kulağa kulak, dişe dişle ve yaralara karşılıklı ödeşme yazdık. Kim hakkından vazgeçerse bu, onun günahlarına keffaret olur. Allah'ın indirdiği ile hükmetmeyenler, işte onlar zalimlerdir.
Tefsirler
Katmanlar
Dersler
Yansımalar
Cevaplar
Kıraat
Hadis
Na tulilifanya ni lazima kwao katika Taurati kwamba mtu huuawa akiua mtu, hutolewa jicho akitoa jicho la mtu, hukatwa pua akikata pua ya mtu, hukatwa sikio akikata sikio la mtu, na hung’olewa jino aking’oa jino la mtu na kwamba hulipizwa kisasi kwa kutia mtu majaraha. Mwenye kusamehe haki yake ya kulipiza kisasi kwa aliyemfanyia uadui, basi huko ni kujifutia na kujiondolea sehemu ya madhambi ya yule aliyefanyiwa uadui. Na yule asiyehukumu kwa yaliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu, katika kisasi na megineyo, basi hao ni wakiukaji wa mipaka ya Mwenyezi Mungu.