The King ˹then˺ said, “Bring him to me.” When the messenger came to him, Joseph said, “Go back to your master and ask him about the case of the women who cut their hands. Surely my Lord has ˹full˺ knowledge of their cunning.”
Tafsirs
Layers
Lessons
Reflections
Answers
Qira'at
Hadith
Mfalme akasema kuwaambia wasaidizi wake, «Mtoeni jela huyo mtu aliyeagua ndoto, na mleteni kwangu.» Yule aliyetumwa na mfalme alipomjia (Yūsuf) kumwita. Yūsuf alisema kumwambia, «Rudi kwa bwanako mfalme umtake awaulize wanawake walioijaruhi mikono yao juu ya uhakika wa mambo yao na habari zao na mimi, ili ukweli ufunuke kwa wote, na kutokuwa na hatia kwangu kuwe wazi, kwani Mola wangu ni Mjuzi zaidi wa mambo waliyoyapanga na waliyoyafanya, hakuna chochote kinachofichika Kwake katika hayo.»