اور وہی ہے جس نے تمہیں زندہ کیا پھر وہ تمہیں موت دے گا پھر تمہیں زندہ کرے گا یقیناً انسان بڑا ہی نا شکرا ہے
تفاسیر
لیئرز
اسباق
تدبرات
جوابات
قرأت
حدیث
Na Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu Aliyewapa uhai kwa kuwafanya mupatikane kutoka kwenye hali ya kutokuwako, kisha Atawafisha umri wenu ukomapo, kisha Atawahuisha kwa kuwafufua ili Awahesabu kwa matendo yenu. Hakika mwanadamu ni mwingi wa kukataa alama zenye kuonyesha uweza wa Mwenyezi Mungu na upweke Wake.