Na kitendo chochote, kichache au kingi, kati ya vitendo vyema yatakayofanywa na kikundi hiki kilichoamini, hakitapotea mbele ya Mwenyezi Mungu. Bali watashukuriwa na watapewa malipo yake. Mwenyezi Mungu Anawajua zaidi wacha-Mungu ambao wametenda mema na wakajitenga na yaliyoharamishwa kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kutaka thawabu Zake.