Na Waliokanusha walisema, «Si hii Qur’ani ateremshiwe Muhammad kwa mara moja» kama ilivyokuwa Taurati, Injili na Zaburi? Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Akasema «Tumeiteremsha ikiwa hivyo, sehemu-sehemu, ili kuutia nguvu moyo wako na ili wewe uzidi utulivu, upate kuielewa na kuibeba, na tumeifunua wazi kwa kuithibitisha na kwa kuileta polepole.»