Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kati yenu na akafanya matendo Aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu , tutampa malipo mema ya matendo yake mara mbili zaidi ya malipo ya asiyekuwa yeye kati ya wanawake wengine, na tumemuandalia yeye riziki nzuri, nayo ni Pepo.