Back to Learning Plan
Kuandaa Mioyo Yetu kwa Ramadhani
Day 4: Kuhifadhi Mioyo Yetu Kupitia Nidhamu Binafsi
Moyo wa mwanadamu, pamoja na mdundo wake, mapigo, na hisia, hubadilika kimwili na kimaumbile. Kitenzi cha Kiarabu: "قَلَبَ," :qalaba (kubadilika) kimeunganishwa moja kwa moja na neno "قَلْبٌ" :qalb (moyo), likionyesha asili ya kubadilika kwa moyo. Kwa maana hii, moyo unaweza kuelekea upande wa huda - mwongozo unaoutajirisha na kuutuliza, au upande wa hawa - tamaa inayouharibu na kuufisha.
Mwenyezi Mungu ametupa mifano ya huda katika Qur’ani, kama vijana wa pangoni waliotajwa katika Surah Al-Kahf, ambao walipoamini, Mwenyezi Mungu akawaongeza katika mwongozo. Hii ni dalili kwamba moyo, ukishikamana na imani, hupewa nguvu ya kusimama imara katika nuru ya uwongofu (huda).
Qur’ani ni huda kwa kuwa huangaza mioyo yetu na kutuongoza katika njia iliyo nyoofu. Nguvu mbili zinazopingana — huda dhidi ya hawa — zimeangaziwa kwa uzuri katika kisa cha Nabii Musa (AS). Qur’ani inasimulia tukio ambapo Musa (AS) alitaka kutafuta nuru katika jangwa lenye giza.
Miongoni mwa mwongozo ambao Mwenyezi Mungu alimpa Musa (AS) katika mlima mtakatifu, kulikuwa na onyo kwamba asije akazuiliwa na wale wanaofuata matamanio yao (hawa) na hivyo kupoteza mtazamo wa Siku ya Kiyama.
Aya hizi zinaonyesha kwamba miongoni mwa mwongozo muhimu zaidi aliopokea Musa (AS) katika mazungumzo yake ya kwanza na Mwenyezi Mungu ni ukumbusho kwamba Saa iko karibu. Kwa hivyo, asikuzuilie yule anayekufuru na kufuata matamanio yake, ukapoteza imani na ukumbusho wa Siku hiyo. Huu ni mwongozo wa Mwenyezi Mungu kwetu sote: kufuata matamanio ya nafsi hututenga na huda Yake na kutupeleka kwenye majuto.
Ramadhani ni fursa kuu ya kuzingatia kile tunachoingiza mioyoni mwetu. Tunaomba tuweze kuchagua mwongozo wa rehema wa Mwenyezi Mungu badala ya matamanio yetu madogo na mara nyingi yenye uharibifu. Katika Ramadhani, kufanya uchaguzi kati ya mwongozo na matamanio huwa rahisi zaidi, kwani tunajizuilia na kujitakasa. Hali ya kiungu inayojengwa na rehema katika msimu huu mtukufu huunda nafasi ya pekee ya kuelekeza nyoyo katika huda (Mwongozo) na kuimarisha imani.
Allah anasema kuhusu Ramadhani:
Mara nyingi ni nafsi yetu ya chini (nafs al-ammārah) inayojitokeza kama kizuizi kinachotuzuia kufuata mwongozo wa Mwenyezi Mungu kwa uthabiti. Ili kupunguza hamu na matamanio yake, ni lazima tuikubali nafsi hii kama sehemu ya utu wetu, lakini tuidhibiti kwa nidhamu ya kila mara. Kwa kufanya hivyo, tunajenga daraja kati ya udhaifu wa nafsi na nuru ya huda.
Mshairi wa Kiarabu Abu Zua'ib al Huzali (aliyefariki mwaka 648 BK) alisema:
وَالنَفسُ راغِبِةٌ إِذا رَغَّبتَها
فَإِذا تُرَدُّ إِلى قَليلٍ تَقنَعُ
"Nafsi ina hamu unapoihimiza; Lakini ukiizuia, itaridhika na kidogo."
والنفس كالطفل إن تهمله شب على
حب الرضـــــاع وإن تفـطمه ينفطــم
"Nafsi ni kama mtoto; ukimpuuza, atakua akipenda kunyonya, lakini ukimwachisha kunyonya, atakua ni mwenye kuwacha."
وجاهد النفس والشيطان واعصهـــما
وإن هما محـــضاك النـــصح فاتــهــم
“Jitahidi kupambana na nafsi yako pamoja na shetani, na uwaasi wote wawili. Na iwapo watakuletea nasaha, basi watilie shaka na uwatuumu.”
فاصرف هواها وحاذر أن تولـــــــــيه
إن الهـــــــــوى ما تولى يصم أو يصــم
“Basi elekeza mbali matamanio yake na jihadhari usiyafuate. Hakika matamanio yakipewa usukani, humfanya mtu kuwa kipofu au kiziwi.”
Kwa kuwa nyoyo zetu huzunguka kati ya mema na mabaya daima, tunaweza kuelekeza nyoyo zetu kwa huda (Mwongozo) ya Mwenyezi Mungu, au kuziacha zishikamanishwe na hawa (matamanio) yenye uharibifu. Nyoyo hujengeka kwa kile tunachozielekeza. Katika mwezi huu wa Sha‘bani, hebu tuzifundishe nyoyo zetu kupokea, kusikiliza, na kutafakari juu ya huda (Mwongozo) bora zaidi — Qur’ani Tukufu.
Je, ni suluhisho gani Qur’ani inatupea kwa tatizo la matamanio?
Jinsi Qur'ani inavyoshughulikia tatizo la matamanio, inaweza kufupishwa kama ifuatavyo:
Kwanza, kupinga mamlaka ya matamanio na kutoyatii. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:
Hapa, msemo 'kusimamishwa mbele ya Mola wake mlezi' unaweza kumaanisha mambo mawili:
Kusimamishwa mbele ya Mwenyezi Mungu kama Muumba Mwenye Nguvu zote anayetuona na kututazama kila tunachofanya.
Kusimamishwa mbele Yake siku ya hesabu, tukitoa maelezo ya matendo yetu.
Kuyakumbuka haya mawili kutatuzuia kutumbukia katika dhambi.
Pili, mwongozo unapaswa kutafutwa kupitia kitabu cha Mwenyezi Mungu, ambacho alikiteremsha kwa Mtume Wake, na kwa kushikamana nacho. Ndani yake kuna kimbilio na utoshelevu wa nafsi dhidi ya matamanio, na humo ndimo mwongozo wa kweli unapatikana. Mwenyezi Mungu anasema:
Tatu, kwa kuwa nafsi huelekea kufuata matamanio yake, Qur’ani inatambua asili hii ya mwanadamu. Hata hivyo, pia inatukataza kujihusisha na kutosheleza matamanio kupita kiasi, ikitukumbusha matokeo mabaya ya kuyafuata. Mwenyezi Mungu anasema:
Yeyote anayefuata matamanio yake, matamanio hayo humpeleka mbali na utiifu kwa Mwenyezi Mungu. Kitendo cha kutotii huathiri moyo, na kuufanya uogope viumbe au mambo mengine badala ya Mwenyezi Mungu. Hii ni aina ya utumwa kwa mwingine asiye Mwenyezi Mungu, na kuchukulia matamanio kama mungu badala Yake.
Soma zaidi kuhusu mada hii kwenye Quranreflect kwa kubofya Tafakari hii (Imechapishwa kwa lugha ya kiingereza)