Back to Learning Plan
Kuandaa Mioyo Yetu kwa Ramadhani
Day 3: Kulinda Mioyo Yetu
Tunalinda mioyo yetu kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu na kutafuta kimbilio Kwake dhidi ya Shetani.
Moyo wa kimwili unalindwa na mbavu, na vivyo hivyo, moyo wa kiroho unalindwa na imani na matendo mema. Haya hufanya kazi kama ngome imara ambayo Shetani daima hujaribu kupenya na kuiharibu. Kwa hivyo, moyo ni sehemu yetu ya thamani zaidi lakini pia dhaifu. Kama wanadamu, tunayo dhamira ya kudhibiti kile tunachoruhusu kuingia ndani ya mioyo yetu. Mara nyingine, tunapopunguza ulinzi wetu, humruhusu adui kuuteka.
Shetani hupenya kupitia milango ya hasira, tamaa, kiburi na wivu. Yoyote kati ya milango hii inaweza kuwa njia ya shambulio, ndiyo maana Qur’ani inatuonya kumchukulia Shetani kama adui wa wazi, aliye tayari kutuvizia.
Qur'ani inatuambia zaidi kwamba njia bora ya kuzuia shambulio kutoka kwa Shetani ni kuepuka kufuata nyayo zake hapo mwanzo. Yeyote anayevutiwa na nyayo zake huwa rahisi kuathiriwa na ushawishi wake kiasi kwamba anapotudanganya tu, nasi tunatii. Mwenyezi Mungu anatukumbusha;
Kwa maneno mengine, tunapaswa kulinda mioyo yetu kama mlinzi aliye macho na anayejua mbinu za adui zake. Hivyo hubaki makini akigundua tishio lolote linaloweza kujitokeza na anaweza kulikabili. Lakini mlinzi anapolegea, huweza kudanganywa na adui yake, akapoteza ulinzi na hatimaye kutekeleza matakwa ya adui huyo. Qur’ani inatuonya wazi: ukifuata nyayo zake, basi Shetani atakuwa na mamlaka zaidi juu yako.
Mwenyezu Mungu Anasema:
Kama vile mlinzi anapohisi tishio huongeza umakini wake, ndivyo muumini anavyopaswa kuwa makini anapohisi mwanzo wa ushawishi wa Shetani. Mioyo yetu ni kama ngome ambayo Shetani hujaribu kupenya na kuharibu kwa kuidhibiti. Tunahitaji kubaki macho, na njia kadhaa za kufanya hivyo ni:
- Kudumu katika hali ya wudhu.
- Kumkumbuka Mwenyezi Mungu kila mara, ili mioyo yetu isibaki na nafasi ya kumridhisha Shetani.
- Kutafuta kimbilio tunapohisi Shetani anajaribu kutushawishi kwa kusoma isti‘ādhah: {أَعُوذُ باللَّهِ مِنَ الشَّيْطاَنِ الرَّجيم} (Natafuta kimbilio kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani aliyelaaniwa). Kama Qur’ani inavyosema: Unaposoma Qur’ani, tafuta kimbilio kwa Mwenyezi Mungu kutokana na Shetani aliyelaaniwa. Hakika hana mamlaka juu ya wale walioamini na wanaomtegemea Mola wao.’ (Qur'ani 16:98-99)
Soma zaidi kuhusu kulinda moyo kwa kubofya Tafakari zifuatazo (zimechapishwa kwa lugha ya kiingereza):