Back to Learning Plan
Kudumisha Mwendo Baada ya Ramadhani
Day 3: Majaribu Yanaporejea
Katika Ramadhani, huwa tunaacha tabia mbaya na dhambi. Lakini sasa Ramadhani imekwisha, huonekana kana kwamba tabia zile za zamani zinatuita turudi. Huenda hata sehemu ya nafsi zetu ilikuwa ikisubiri kwa hamu kurejea katika tabia hizo mara Ramadhani itakapofikia tamati.
Changamoto huongezeka kwa sababu shaytani sasa ameachiwa tena kutujaribu na kutushawishi kurejea katika dhambi. Lakini tusiuone mwisho wa Ramadhani kama ishara ya kurudi katika mwenendo wa zamani.
Badala yake, tuuone kama mwanzo mpya — fursa ya kuendelea kukua, kujiboresha, na kudumisha nidhamu tuliyojenga.
Kumbuka nidhamu uliyokuwa nayo katika Ramadhani, hata kutokunywa tone moja la maji wakati kiu ilipokuwa kali. Shikilia nguvu hiyo unapokabiliana na changamoto za ndani na za nje zilizo mbele yako. Majaribu yanapotuzingira, kumbuka dua ambayo Allah ametufundisha ya kuomba msaada Wake ili tusikengeuke na kuangukia katika dhambi:
Allahumma Ameen!
Jilinde Dhidi ya Majaribu
Tunapokabiliwa na majaribu, ni lazima tukumbuke kumwomba Allah hifadhi dhidi ya shetani na kumuomba msaada Wake. Lakini pia ni jukumu letu kulinda nafsi zetu kwa kuchukua hatua za makusudi kuepuka hali au mienendo inayoweza kutupotosha. Sambamba na kuwa makini na kutambua majaribu yanayotuvuta kuelekea kutenda dhambi pamoja na mazingira yanayochochea tabia mbaya.
Qur’ani inaweka wazi kwamba shaytani hana mamlaka juu ya wale wanaoamini na wanaomtegemea Allah.
.Iwapo unajua kwamba kundi fulani la marafiki lina tabia ya kusengenya na kuzungumza vibaya kuhusu wengine, ili kuepuka kuhusika katika hilo, unaweza kupunguza hatari ya kuangukia katika mtego wa kusengenya kwa kuwa muwazi na mkweli kuhusu mienendo hiyo na jinsi inavyokuathiri.
Ikiwa programu fulani ya simu zinakusababisha kuteleza na kuangukia katika majaribu, zifute na tafuta mbadala zisizoathiri vibaya moyo wako.
Na iwapo kukaa usiku kucha kwenye simu, kula vyakula visivyo na afya, au kutazama Netflix kunakusababisha kukosa Swala ya Alfajiri, basi dhibiti hilo kwa kuepuka au kuweka mipaka madhubuti kwenye vichocheo hivyo.
Kwa kutambua ushawishi huu, tunaweza kuchukua hatua za kuyaondoa katika maisha yetu kadri iwezekanavyo, huku tukijitahidi kuyabadilisha kwa tabia na mazingira bora zaidi. Tuchukue mfano kutoka katika maisha ya Nabii Yusuf (amani iwe juu yake), aliyegundua kwamba njia pekee ya kuondokana na majaribu ni Allah kumuondoa katika mazingira ya majaribu. Hili linaonekana katika dua aliyosema:
Kuwa Mwepesi wa Kurejea Kwake
Ikiwa tutajikuta tukirejea katika tabia za zamani, tukumbuke kumrudia Allah haraka, tusije tukazoea au kupuuzia kumuasi Allah SWT. Allah (Aliyetukuka, Aliye juu kabisa) anasema:
Ili kuhakikisha dhambi zetu zinabadilishwa na matendo mema, haitoshi kutubia tu. Bali pia tunaweza kufuatisha kosa kwa tendo jema, kama kuswali rakaa mbili za swala za hiari. Allah SWT (Aliyetukuka, Aliye juu kabisa) anasema:
Vivyo hivyo, kutoa sadaka baada ya kufanya dhambi hututakasa na dhambi hizo. Allah anasema:
Allah anatupa uhakika kwamba bila shaka Yeye anakubali toba zetu na anapokea sadaka zetu: