Back to Learning Plan
Kudumisha Mwendo Baada ya Ramadhani
Day 1: Tafakari Kuhusu Ramadhani
Fikiria unajenga nyumba, kwa kutumia chokaa na matofali, unapanga kila chumba, na kupamba ndani na nje yake, kisha ghafla unaiacha. Bila shaka, hili lingekuwa jambo lisilo na manufaa. Vivyo hivyo, katika Ramadhani, tuliswali qiyam (swala ya usiku), tukafunga mwezi mzima, na kujenga tabia njema kwa lengo la kujenga taqwa (uchamungu kwa Allah)—nyumba yetu ya kiroho. Sasa si wakati wa kubomoa mema tuliyokusanya kwa kuacha mafundisho ya Ramadhani na kuiacha nyumba hii.
Allah anatukumbusha katika Qur’ani kwamba Ramadhani ilikuwa ni mazoezi ya muda mfupi yaliyokusudiwa kutuachia manufaa ya maisha yote. Allah anasema:
Allah anaeleza matokeo ya muda mrefu ya kufunga, nayo ni uchanmngu zaidi kwa Allah. Kusudi hili halikomei Ramadhani pekee, bali hisia yetu mpya ya uchamungu inapaswa kuendelea katika maisha yetu yote na katika hali zote, ikitusaidia kutekeleza wajibu wetu kama Waumini katika kutafuta radhi za Allah.
Qur’ani inatukumbusha kuwa kuwa na taqwa ni safari ya maisha yote, na tunapaswa kufa katika hali ya kujisalimisha.
Tena, Allah anaeleza kwamba matokeo ya muda mrefu ya kufunga ni uchamngu zaidi kwa Allah. Kusudi hili halina mipaka ya Ramadhani; uchamungu wetu uliorejewa unapaswa kuendelea bila kikomo, ukitusaidia kutimiza wajibu wetu kama Waumini katika kutafuta radhi za Allah.
Anza na Shukrani
Allah anatukumbusha kuwa lengo jingine la Ramadhani ni kupandikiza ndani yetu hisia ya shukrani:
Tuanze safari yetu ya baada ya Ramadhani kwa shukrani kwa Allah. Lazima tutambue na kuthamini neema nyingi tulizopewa kwa ujumla, na hasa katika mwezi huu mtukufu: fursa ya kutakasa miili na roho zetu kupitia kufunga na ibada, nyakati za uwazi wa moyo na amani ya ndani, kuongezeka kwa taqwa, hadi neema ya chakula na maji ya kufuturu. Simama kidogo uwafikirie wale ambao hawajawahi kuonja furaha na manufaa ya Ramadhani, na wanakosa baraka zake kabisa, bila hata kujua kuwepo kwa Laylatul Qadr! Na pia wafikirie waliopitia hali ngumu sana, waliong’olewa makwao, wakapoteza mengi, wakanyimwa mahitaji ya msingi katika mwezi huu mtukufu, ilhali bado walifunga Ramadhani. Ni wajibu wetu kumshukuru Allah kwa neema tulizopokea, na kuendelea kuwaunga mkono wanaoteseka na kuwaombea dua hata baada ya Ramadhani.
Kutafuta Kutakabaliwa
Neno “Tutakabalie” katika aya hii, kwa Kiarabu taqabbul, linaashiria kitendo cha kuwasilisha jambo kwa unyenyekevu kwa Mola wetu na kuomba likubaliwe, licha ya upungufu wake. Aya hii inahusiana na dua ya Nabii Ibrahim na Ismail (amani iwe juu yao) baada ya kujenga upya Ka‘bah. Imam Al-Razi anaeleza kwamba kuomba kukubaliwa kunaonyesha jitihada ya dhati ya mja katika kutafuta radhi za Allah, hasa pale ambapo tendo lina mapungufu. Ni kukiri udhaifu wetu na kujisalimisha kwetu.
Tafakari matendo na nia zako katika Ramadhani. Je, ulitekeleza wajibu wako kwa ikhlasi? Omba msamaha kwa mapungufu yoyote. Fanya dua ya dhati ukimuomba Allah akubali kufunga kwako, swala zako, sadaka zako na matendo mema.
Huenda tulianza Ramadhani kwa motisha kubwa, lakini katikati tukalegea. Pengine tulipunguza umakini katika swala au dhikr. Kuomba Allah ayakubali matendo yetu licha ya dosari zake ni kumuomba ayapokee kwa rehema Yake, si kwa ubora wa matendo yetu.
Kamilisha kwa kuomba msamaha baada ya kila tendo jema.
Aya ya 73:20 inatukumbusha tusijione wakamilifu baada ya kufanya mema, bali tumuombe Allah msamaha, kama ishara ya unyenyekevu na ikhlasi. Tunaona pia agizo kama hilo kwa Mtume (rehema na amani zimshukie) baada ya ushindi wa Makkah:
Zakatul Fitr imefananishwa na sajdah ya sahw. Kama sajdah hiyo inavyorekebisha makosa ya swala, Zakatul Fitr inarekebisha mapungufu ya ibada za Ramadhani. Na hata baada ya Ramadhani, tuendelee kutoa sadaka kama utakaso wa nafsi na kuziba mapengo ya ibada zetu.
Kutathmini Ukuaji wa Kiroho
Tafakari maendeleo yako ya kiroho katika Ramadhani. Huenda ulijenga tabia bora, ukaongeza maarifa ya dini, au ukaimarisha uhusiano wako na Allah. Fikiria nini kilichochangia maendeleo hayo na jinsi ya kuyadumisha. Kama unahisi ungeweza kufanya zaidi, tafakari maeneo ya kuboresha. Ni vikwazo gani vilikuwepo? Weka malengo halisi ya ukuaji wa kiroho baada ya Ramadhani, na anza kujenga tabia sasa ili ufikie Ramadhani ijayo ukiwa na imani iliyo juu zaidi.
Tutazungumzia hili kwa undani zaidi katika somo lijalo.
Kuanza Sura Mpya
Ingawa Ramadhani hii imekwisha, fursa ya kukua haijaisha. Nafasi ya kuimarisha uhusiano wetu na Allah ipo hadi pumzi ya mwisho.
Allah SWT anatukumbusha:
Kama alivyosema Al-Raghib Al-Asfahani, jihadi ni kutumia jitihada zote katika kupambana na adui (اسْتِفْراغُ الوُسْعِ في مُدافَعَةِ العَدُوِّ). Adui mkubwa kwetu ni matamanio, tamaa na nafsi. Ramadhani hutupatia mazingira bora ya kuyadhibiti, lakini mapambano yanaendelea hata sasa.
Kila wakati ni fursa ya kujikaribisha kwa Allah. Tuchukue mafunzo ya Ramadhani kwa shukrani, tutafute kukubaliwa, na tujitahidi kuendelea kuboresha imani na matendo yetu. Allah atujalie nguvu, uongofu na uthabiti katika njia iliyonyooka. Ameen.
Kufunga Ndio Mwanzo wa Uthabiti
Andika tabia njema ulizojenga Ramadhani na jinsi utakavyozidumisha hadi Ramadhani ijayo. Jiulize: “Ni nini kilinichochea?” Kisha jiulize: “Nitadumishaje motisha hiyo daima?”
Kumbuka kuwa kumuabudu Allah na kutafuta radhi Zake kunahitaji subira na uthabiti:
Sufyan bin Abdullah (Allah amridhie) amesimulia:
“Nilisema, ‘Ee Mtume wa Allah, niambie jambo moja kuhusu Uislamu ambalo sitamuuliza mtu mwingine.’ Akasema, ‘Sema: Ninaamini kwa Allah, kisha uwe thabiti.’” (Muslim)
Unakaribishwa kushiriki tafakari zako za Ramadhani na kushirikiana na wengine katika QuranReflect kwa kutumia alama ya reli #RamadanTaughtMe.