Back to Learning Plan
Lenzi Tano za Kutafakari Qur’ani
Day 3: Kichujio cha Moyo
“Ni nini kinachonizuia kuitafakari Qur’ani?”
Jambo kubwa linalowazuia watu wengi kutafakari Qur’ani kwa vitendo ni hofu ya kukosea. Nataka kukuambia kwamba hii ni hofu nzuri, inayotokana na heshima na taadhima kwa Maneno ya Mwenyezi Mungu.
Tunataka kudumisha taadhima hiyo na heshima hiyo nzuri kwa mipaka yetu wenyewe. Lakini pia tunapaswa kuzuia hofu isije ikawa kizuizi cha kujenga uhusiano wa maana na Qur’ani.
“Je, ninahitaji kuwa mwandishi mwenye kipaji ili kutafakari Qur’ani?”
Hapana. Hakuna anayekuomba uandike makala ya kuvutia inayofafanua aya, au kuja na nadharia ya kushangaza akili. Tafakari inaweza kupelekea mambo kama hayo, lakini lengo kuu ni rahisi sana: kuiruhusu Qur’ani kugusa moyo wako na iwe na athari katika maisha yako.
Kumbuka kwamba Kitabu hiki, kabla hakijafikishwa kwetu, kiliteremshwa juu ya MOYO wa Mtume (rehema na amani zimshukie).
Kwa hiyo, na tuwe wazi tangu mwanzo kwamba tafakari (tadabbur) SI zoezi la kiakili pekee.
“Kichujio cha moyo ni nini?”
Kabla ya kuzifafanua zile Lenzi Tano za uchambuzi, tunapaswa kutambua kwamba kuna kichujio ambacho kila kitu kitapitia. Kichujio hicho ni moyo. Kama vile tabaka la rangi linavyoathiri lenzi ya kamera au kioo cha kukuza, vivyo hivyo Kichujio cha Moyo “hupaka rangi” mtazamo wako juu ya Maneno ya Mwenyezi Mungu kulingana na “rangi” iliyopo ndani ya moyo wako.
Baada ya yote, wapo watu wanaoisikia Qur’ani au hata kuisoma kama taaluma yao, lakini hawapati lishe ya kiroho, wala uongofu au mabadiliko ya nafsi. Wao ni kama wale waliotajwa katika Qur’ani, wanaouliza kwa nia isiyo ya dhati:
[Hapa kuna tafakari yenye kugusa sana juu ya aya hiyo, iliyoandikwa kutokana na hali mpya na ya kutisha ambayo wengi wetu tuliushuhudia wakati wa Covid-19:
quranreflect.com/posts/2777] (kwa lugha ya kiingereza)
“Kichujio cha moyo kinamaanisha nini kwa muumini?”
Kwa waumini, hii inamaanisha kusafisha nyoyo zetu ili kupokea mwanga wa mwongozo. Tunayakaribia Maneno ya Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu na umakini.
Na muhimu zaidi, ni lazima tuendelee kuusafisha na kuutakasa moyo huu (ikiwemo kupitia kusoma Qur’ani na tafakari), ili uendelee kutuonyesha Qur’ani kama ilivyo, na kama ilivyokusudiwa ionekane.