Back to Learning Plan
Lenzi Tano za Kutafakari Qur’ani
Day 2: Ninaanzaje Kutafakari Qur’ani?
“Kuna tofauti gani kati ya tadabbur na tafsiri?”
Kuna mkanganyiko mkubwa kuhusu maana halisi ya kutafakari Qur’ani, jambo ambalo kwa Kiarabu mara nyingi huitwa TADABBUR.
Tunajua kwamba TADABBUR si sawa na TAFSIR. Tafsir ni taaluma ya kielimu inayohusisha kufafanua maana za Qur’ani. Hakuna aya katika Qur’ani inayowaamuru watu wote kufanya tafsir, lakini kuna aya nyingi zinazosisitiza umuhimu wa tadabbur.
“Ni nani anayepaswa kutafakari Qur’ani?”
Tafakari ni kwa ajili ya kila mmoja wetu — kuanzia mwanazuoni mkubwa kabisa hadi mimi na wewe. Ni njia ya kuipokea Qur’ani kwa umakini wa akili na wa moyo, na kuruhusu ujumbe wake utuathiri.
Sio swali la:
“Qur’ani inamaanisha nini?”
bali ni:
“Hii aya inamaanisha nini katika maisha YANGU?”
“Hii aya Ina umuhimu gani katika maisha YANGU?”
“Nitafichua nini ninapotafakari?”
Kutafakari huanza kwa kuangalia mwonekano dhahiri wa aya, kisha kuzama ndani zaidi. Wakati huo huo, tafakuri humaanisha pia kuzama ndani ya nafsi zetu.
Katika pande zote mbili — ndani ya Qur’ani na ndani ya nafsi — tunafichua ukweli ambao pengine tulikuwa tunaujua tayari, lakini tulihitaji kuuthamini na kuukumbuka upya.
Hili ni tendo la uaminifu wa imani linaloanza kwa yakini kamili kwamba haya ni maneno ya Muumba wangu, Mola wangu na Mwelekezi wangu. Hakuna upotovu katika maneno Yake, wala hakuna chochote kilichopo bila hekima kamilifu.
“Je, itakuwaje kama mimi si mzuri katika kutafakari?”
Soma tafakari nzuri (ya kiingereza) kuhusu aya hii hapa:
“Fake it ’til you Make it”
Ili tujinyenyekeze na kuruhusu Wahyi utubadilishe, tunahitaji kukuza ujuzi wa tafakuri. Huu si ujuzi wa kuzaliwa nao tu, bali ni jambo la kujifunza na kulilea. Ni aina ya uelewa unaozidi ule wa herufi na sauti.
Hivyo basi, tutakuwa tukizingatia maana na athari zake, na kozi hii itakuletea muhtasari wa stadi muhimu kwa mfumo wa Lenzi Tano. Ukishajua kuzitumia, unaweza kuanza katika kiwango cha msingi kabisa na kupanda hatua kwa hatua.
“Lenzi hizi tano ni zipi?”
Tunao Lenzi ya:
Maneno (yaliyotumika au hayakutumika)
Ulimwengu wa Qur’ani
Uzoefu Binafsi
Miunganiko (kati ya ayah au sura za Qur'ani)
Mafunzo ya Jumla
Lakini kabla hatujafika huko, kuna jambo muhimu sana la kushughulikia katika somo linalofuata… basi endelea kuwa nasi.