Sign in
Sign in
Sign in
Select Language

Back to Learning Plan

Mwokozi: Masomo yenye Athari Kubwa Kutoka Surah Al-Mulk

1: Mfalme wa Wafalme Wote
2: Ukamilifu wa Uumbaji Wake
3: Onyo Ambalo Hatuwezi Kulipuuza
4: Yule Anayekujua Zaidi
5: Ardhi Iliyo Chini ya Miguu Yako
6: Mafunzo Kutoka kwa Waliokataa Ukweli
7: Kabla Maji Kudidimia Ardhini

Back to Learning Plan

Mwokozi: Masomo yenye Athari Kubwa Kutoka Surah Al-Mulk

Day 3: Onyo Ambalo Hatuwezi Kulipuuza

Mada: Hatima ya wale wanaopinga ishara za Allah

Aya za Qur’ani

Somo na Tafakari

Aya hizi zinachora picha ya Akhera iliyo dhahiri na ya kutisha kwa wale wanaompinga Mwenyezi Mungu, wajumbe Wake na ujumbe Wake kimakusudi. Hii si maelezo ya kawaida hata kidogo. Imekusudiwa kuamsha mioyo iliyo lala katika usingizi wa dhana potofu. Jahannamu inasifiwa kana kwamba inanguruma, na kuchemka, na karibu kupasuka kwa hasira iliyo nayo. Haya si maneno ya hadithi ya mbali; ni maneno ya Yule aliyeumba Pepo na Jahannamu, akituambia waziwazi: hili ni kweli, na liko karibu.

Angalia swali ambalo malaika wa Jahannamu wanauliza: "Je, mwonyaji hakukujieni?" Hili si swali la kumjuza Mwenyezi Mungu; tayari anajua! Bali ni changamoto kwao wenyewe, kuwa wamepewa ishara lakini hawakugeuka. Hawawezi kusema hawakuwa na taarifa. Manabii walikuja. Mitume walizungumza. Qur'ani iliteremshwa. Na katika zama zetu, ukumbusho bado unatufika kupitia adhina ya sala, kusikika kwa Qur’ani, ushauri wa rafiki, na hata minong'ono ya dhamiri mioyoni mwetu.

Msiba mkuu si ujinga bali ni kutojali. Watu walisikia lakini hawakutenda. Waliona ishara lakini walizipuuza. Katika dunia, kupuuza onyo kunaweza kukugharimu pesa, afya, au fursa. Lakini katika Akhera, kupuuza onyo la Mwenyezi Mungu kunaweza kukugharimu furaha ya milele.

Na bado, hata katika onyo hili, kuna rehema isiyotamkwa. Aya hizo zimeteremshwa wakati bado sisi tuko duniani (kabla ya matukio hayo kutendeka), huku milango ya toba ikiwa bado imefunguliwa. Ikiwa tunahisi hofu tunaposoma aya hizi, basi hiyo ni neema kubwa maana hofu kabla ya kifo ni ishara ya usalama baada yake. Hatari halisi ni moyo ambao hauhisi chochote.

Kiini cha Jambo: Jahannamu si dhana tu. Ni mahali ambapo Mwenyezi Mungu anatuonya tujilinde nayo sasa, ili mtu yeyote asifike huko kwa mshangao. Kuyachukua maonyo haya kwa uzito ni kuipa thamani ya kweli roho zetu. Mwenyezi Mungu hamshangazi mtu yeyote kwa adhabu; Anampa kila mtu nafasi ya kurudi nyuma na kuzingatia. Kama Anavyosema katika Qur’ani:
“(Mwenyezi Mungu) asema: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.” (Qur'ani 50:28)

Hadith ya Mtume (Rehema na amani zimshukie)

Mtume (Rehema na amani zimshukie) amesema:
“Pepo imezungukwa na taabu, na Moto imezungukwa na matamanio.”
(Sahih Muslim, Hadith 2822)

Usisome tu, bali tenda…

Leo, chagua dhambi moja (hata ndogo) ambayo umekuwa ukichelewesha toba, kisha utubu kwa ajili ya Allah. Sema kwa dhati: Ee Mwenyezi Mungu, naiacha dhambi hii kwa sababu naogopa hasira Yako na natumaini rehema Yako.

Jinsi inavyosaidia:

  • Hubadilisha hofu kuwa kitendo.
  • Huimarisha udhibiti wa nafsi (nafs) yako na kujizuia.
  • Hufungua moyo kwa msamaha wa Allah.

Dua

اللَّهُمَّ أَجِرْنِي مِنَ النَّار

Allāhumma ajirnī min an-nār.
“Ee Mwenyezi Mungu, nilinde kutokana na Moto.”
(Sunan Abi Dawud, Hadith 5079)

Tafakari hili:

Ikiwa malaika wa Jahannamu wangekuuliza leo: “Kwani hakukujieni mwonyaji?”, ni ushahidi gani kutoka maishani mwako ungethibitisha jawabu lako?

Add Reflection

Stay Connected to the Quran ❤️

Short meaningful reminders to reset, reflect and stay connected to the Quran.

Read, Listen, Search, and Reflect on the Quran

Quran.com is a trusted platform used by millions worldwide to read, search, listen to, and reflect on the Quran in multiple languages. It provides translations, tafsir, recitations, word-by-word translation, and tools for deeper study, making the Quran accessible to everyone.

As a Sadaqah Jariyah, Quran.com is dedicated to helping people connect deeply with the Quran. Supported by Quran.Foundation, a 501(c)(3) non-profit organization, Quran.com continues to grow as a free and valuable resource for all, Alhamdulillah.

Navigate
Home
Quran Radio
Reciters
About Us
Developers
Product Updates
Feedback
Help
Donate
Our Projects
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Quran.AI
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Non-profit projects owned, managed, or sponsored by Quran.Foundation
Popular Links
Duas from the Quran
Quran Verse of the Day
Ayatul Kursi
Yaseen
Al Mulk
Ar-Rahman
Al Waqi'ah
Al Kahf
Al Muzzammil
SitemapPrivacyTerms and Conditions
© 2026 Quran.com. All Rights Reserved
Contribute