Back to Learning Plan
Uraibu wa Skrini: Skrini Zinapouiba Moyo
Day 2: Muda ni Amana
Aya za Qur’ani
Somo na Tafakari
Tunaishi katika zama ambazo skrini hazili tu muda wetu, bali pia mioyo yetu, umakini, na utulivu wetu. Simu imekuwa rafiki wa kudumu—mara nyingi zaidi kuliko watu, kuliko swala, na kuliko kusudi letu la kweli la kuwa waja wa Ar-Rahman. Kutazama na kupitia skrini hakuishi, na cha kusikitisha ni kwamba taratibu tunapoteza umakini, tunadhoofisha mahusiano, na tunasahau kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Kila wakati ni uwekezaji au deni; thawabu zake tutazikuta kwa Mola wetu, au ni deni tutakalohesabiwa. Kwa hiyo, ni lazima tuchague kwa hekima na kwa kusudi jinsi tunavyoutumia muda wetu.
Katika Surah Al-Mulk (67:23), Mwenyezi Mungu anatukumbusha kwamba Yeye ndiye aliyetuweka katika uhai na akatupatia hisia zetu—masikio, macho, na akili—lakini uhalisia ni kwamba wengi ni wazembe na hawashukuru kwa neema hizi zisizopimika. Kumshukuru Muumba wetu si kwa maneno pekee, bali kwa kutumia neema hizi kwa namna inayoakisi shukrani ya kweli. Kuweka hisia zetu katika maudhui yenye manufaa—kama usomaji wa Qur’ani au kutafuta elimu yenye faida—ni aina ya shukrani. Kinyume chake, kutumia vibaya hisia zetu kufuata matamanio ya upuuzi au kujitumbukiza katika burudani kupita kiasi si tu kupoteza muda, bali ni khiyana ya amana aliyotuwekea. Shukrani ya kweli huonyeshwa kwa matumizi ya makusudi na yenye nia ya kile tulichojaaliwa, tukilinganisha matendo yetu na kusudi ambalo vipawa hivi viliumbwa kwa ajili yake.
Surah Al-Baqarah inaonya dhidi ya kujiangamiza. Kupoteza muda si jambo lisilo na athari. Huharibu roho, hukutenganisha na Mwenyezi Mungu, na huongeza usumbufu. Muda uliopotea hauwezi kurejeshwa. Wema, kwa upande mwingine, ni juhudi zilizoelekezwa kwa kusudi—iwe ni kumkumbuka Mwenyezi Mungu, kuwahudumia wengine, kutafuta elimu, au kupumzika kwa nia njema. Nia njema kabla ya tendo lolote, hata la kawaida, hufanya muda huo uwe umetumika vyema.
Utaulizwa ulivyotumia ujana wako, afya yako, na muda wako wa ziada. Uraibu wa skrini mara nyingi hujificha nyuma ya kauli ya “video moja tu zaidi.” Lakini kila wakati, ima unakusogeza karibu na Mwenyezi Mungu au unakutenganisha Naye.
Hadithi ya Mtume (rehema na amani zimshukie)
Nabii Muhammad (rehema na amani zimshukie) alisema:
“Miguu ya mja wa Mwenyezi Mungu haitasogea Siku ya Kiyama mpaka aulizwe kuhusu mambo matano: kuhusu maisha yake na alivyo yatumia, kuhusu elimu yake na alichofanya nayo, kuhusu mali yake alivyopata na alivyotumia, na kuhusu mwili wake alivyoutumia.”
(Jāmi‘ at-Tirmidhī, Hadithi 2417)
Kipengele cha pamoja katika mambo haya yote yaliyotajwa katika hadithi hii ni muda—uliutumiaje? Maisha ni mkusanyiko wa nyakati; elimu inahitaji muda ili kupatikana na kusambazwa, na mali pia. Hata juhudi za mwili ni matumizi ya muda. Muda ni sarafu isiyoonekana tunayoibadilisha kila wakati kwa manufaa ya dunia. Lakini ubadilishanaji bora zaidi ni ule unaofanywa kwa kuzingatia Akhera.
Usisome tu, bali tenda…
Ukaguzi wa Muda: Chagua saa moja leo bila skrini. litumie katika jambo lenye maana kama kuswali, kutembea, kusoma Qur’ani, au kumsaidia mtu. Angalia jinsi linavyoathiri amani na umakini wako.
Dua
“Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie nitumie muda wangu kwa njia zinazokupendeza. Usiruhusu hata wakati mmoja upite katika uzembe, na ifanye kila siku iwe hatua ya kunikaribisha Kwako.”
Tafakari hili
Kama ningejua kwamba mwishoni mwa leo nitaulizwa jinsi nilivyoitumia siku yangu, ningeitumiaje?
Vivyo hivyo, nikijua kwamba nitaulizwa jinsi nilivyotumia siku zangu zote katika maisha yangu, je, ufahamu huu unaathirije ratiba yangu, na utaathiri vipi kuanzia sasa namna ninavyoutumia muda wangu?